This website uses cookies to ensure you get the best experience on our website.
Maswali na Majibu ya sauti za Kiswahili

1. Dondoa sauti mwambatano zilizo kwenye maneno haya kisha utaje mahali pa kuzitamkia;

       i) ngao /ng/- kaakaa laini

       ii) avya /vy/- meno

2. Tambua muundo silabi katika neno MAKTABA

          KIKKIKI

3. Eleza sifa mbili mbili za sauti zifuatazo 

/i/ 

-Irabu ya mbele ya ulimi/hutamkiwa mbele ya ulimi.

- Inapotamkwa midomo hutandaza.

/o/

- Irabu ya nyuma ya ulimi / hutamkiwa nyuma ya ulimi.

- Inapotamkwa midomo huviringa.

4. Onyesha mahali mkazo unapowekwa kwenye neno ‘Tenganisha’

– Tenga‘nisha/ tenganisha

5. Eleza matumizi manne ya kiimbo.

– Kutolea rai/wazo

- Kuuliza swali.

- Kuonyesha amri/kuamrisha.

- Kuonyesha mshangao.

6. Andika tofauti mojamoja kati ya sauti. 

   /ny/ na /y/

/ny/ ni king’ong’o ilhali /y/ ni kiyeyusho/nusu irabu

   /g/ na /gh/

 /g/ ni kipasuo ilhali /gh/ ni kikwamizo.

7. Andika tofauti moja kati ya sauti zifuatazo

i. /ny/ na /y/

 /ny/ ni king’ong’o ilhali /y/ kiyeyusho

ii. /d/ na /t/

 /d/ ni ghuna ilhali /t/  sighuna

iii. /mb/ na /nd/

 /mb/ ni sauti ya midomo ilhali /nd/ ni ya ufizi

iv. /s/ na /z/

/s/ ni sighuna ilhali /z/ ni ghuna

8. Taja sifa moja linganishi kwa sauti /t/ na /l/.

-Ni sauti za ufizi.

9. Huku ukitoa mifano, eleza miundo miwili ya silabi mwambatano

i)KKI-nyumba

ii)KKKI-mbweha

Andika neno lenye sifa zifuatazo; Kipasuo ghuna cha ufizi, irabu ya kati, kipasuo sighuna cha ufizi, irabu itamkwayo midomo ikiwa imetandazwa

-data

10. Taja sauti zifuatazo:

i) Kikwamizo sighuna cha ufizi (alama 1)

/s/

ii) Nusu irabu ya kaakaa gumu (alama 1)

/y/

11. Ni sauti gani haifai kuwa miongoni mwa hizi. Toa sababu (alama 2)

i. /ng’/ /g/ /t/ /k/

Sauti /ng’/ ni king’ong’o ilhali zingine ni vipasuo

ii. /s/ /v/ /ch/ /sh/

Sauti /ch/ ni kizuio kwamizwa ilhali izingine ni vikwamizo

12. Taja sauti zilizo na sifa zifuatazo: (Alama 2)

(i) sauti ya wastani na nyuma ya ulimi

/o/

(ii) kikwamizo cha ufizi

/z/

(iii) hutamkiwa koromeo

/h/

(iv) hutamkwa ncha ya ulimi inapojipigapiga haraka kwenye ufizi

/r/

13. Andika neno lenye sauti zifuatazo (alama 1)

Kipasuo-kwamizo sighuna cha kaakaa gumu,irabu ya juu,nyuma,irabu ya juu,nyuma ,kikwaruzo ghuna cha masine,irabu ya chini,kati tandaze 

-chuuza

14. Dondoa sauti mwambatano katika maneno yafuatayo na uainishe mahali pa kutamkia. (alama 1)

Tamba 

/mb/ midomo

Afya

/fy/ midomo-meno

15. Linganua irabu katika neno; mavue. (alama 1) 

/a/ chini, kati tandazi

/u/ sauti ya nyuma juu virigwa

/e/ sauti ya mbele wastani, tandazi