Maswali na Majibu ya sauti za Kiswahili

1. Dondoa sauti mwambatano zilizo kwenye maneno haya kisha utaje mahali pa kuzitamkia;

       i) ngao /ng/- kaakaa laini

       ii) avya /vy/- meno

2. Tambua muundo silabi katika neno MAKTABA

          KIKKIKI

3. Eleza sifa mbili mbili za sauti zifuatazo 

/i/ 

-Irabu ya mbele ya ulimi/hutamkiwa mbele ya ulimi.

- Inapotamkwa midomo hutandaza.

/o/

- Irabu ya nyuma ya ulimi / hutamkiwa nyuma ya ulimi.

- Inapotamkwa midomo huviringa.

4. Onyesha mahali mkazo unapowekwa kwenye neno ‘Tenganisha’

– Tenga‘nisha/ tenganisha

5. Eleza matumizi manne ya kiimbo.

– Kutolea rai/wazo

- Kuuliza swali.

- Kuonyesha amri/kuamrisha.

- Kuonyesha mshangao.

6. Andika tofauti mojamoja kati ya sauti. 

   /ny/ na /y/

/ny/ ni king’ong’o ilhali /y/ ni kiyeyusho/nusu irabu

   /g/ na /gh/

 /g/ ni kipasuo ilhali /gh/ ni kikwamizo.

7. Andika tofauti moja kati ya sauti zifuatazo

i. /ny/ na /y/

 /ny/ ni king’ong’o ilhali /y/ kiyeyusho

ii. /d/ na /t/

 /d/ ni ghuna ilhali /t/  sighuna

iii. /mb/ na /nd/

 /mb/ ni sauti ya midomo ilhali /nd/ ni ya ufizi

iv. /s/ na /z/

/s/ ni sighuna ilhali /z/ ni ghuna

8. Taja sifa moja linganishi kwa sauti /t/ na /l/.

-Ni sauti za ufizi.

9. Huku ukitoa mifano, eleza miundo miwili ya silabi mwambatano

i)KKI-nyumba

ii)KKKI-mbweha

Andika neno lenye sifa zifuatazo; Kipasuo ghuna cha ufizi, irabu ya kati, kipasuo sighuna cha ufizi, irabu itamkwayo midomo ikiwa imetandazwa

-data

10. Taja sauti zifuatazo:

i) Kikwamizo sighuna cha ufizi (alama 1)

/s/

ii) Nusu irabu ya kaakaa gumu (alama 1)

/y/

11. Ni sauti gani haifai kuwa miongoni mwa hizi. Toa sababu (alama 2)

i. /ng’/ /g/ /t/ /k/

Sauti /ng’/ ni king’ong’o ilhali zingine ni vipasuo

ii. /s/ /v/ /ch/ /sh/

Sauti /ch/ ni kizuio kwamizwa ilhali izingine ni vikwamizo

12. Taja sauti zilizo na sifa zifuatazo: (Alama 2)

(i) sauti ya wastani na nyuma ya ulimi

/o/

(ii) kikwamizo cha ufizi

/z/

(iii) hutamkiwa koromeo

/h/

(iv) hutamkwa ncha ya ulimi inapojipigapiga haraka kwenye ufizi

/r/

13. Andika neno lenye sauti zifuatazo (alama 1)

Kipasuo-kwamizo sighuna cha kaakaa gumu,irabu ya juu,nyuma,irabu ya juu,nyuma ,kikwaruzo ghuna cha masine,irabu ya chini,kati tandaze 

-chuuza

14. Dondoa sauti mwambatano katika maneno yafuatayo na uainishe mahali pa kutamkia. (alama 1)

Tamba 

/mb/ midomo

Afya

/fy/ midomo-meno

15. Linganua irabu katika neno; mavue. (alama 1) 

/a/ chini, kati tandazi

/u/ sauti ya nyuma juu virigwa

/e/ sauti ya mbele wastani, tandazi