Maswali na majibu ya Nguu za Jadi

9. ‘Habari hizo nimeshazipata tangu juzi. Mwakala wangu hawalali. Wala hayo yasikutie tumbo joto’
a) Weka dondo hili katika mukthadha wake (alama 4)

1. a) 'Mimi ni mwanamume. Ninaweza kuoa wakati wowote na idadi yoyote ya wanawake. Shida iko wapi'? Mwanamke akishaolewa, basi. Yake yamekwisha hapo. Azae na kuitumikia jamaa yake bila kuulizauliza maswali.'

i. Weka dondoo hili katika muktadha wake.

ü  Ni maneno ya Mrima.

ü  Anamjibu Mangwasha mkewe.

ü  Wako nyumbani kwao.

ü  Mangwasha almuulza ikiwa Sagilu anamtafutia mkc mwingine kisiri

ii. Fafanua sifa sita za msemaji wa maneno haya. (alama 6)

Mrima

ü  Mtamaduni- anasema mila hairubusu ycye akatunzwe na mkc kama ngonjwa.

ü  Mbadhirifu- anafuja pesa na mwanamkc njc ya ndoa.

ü  Mzinzi- ana mwanamke nje ya ndoa- kutoka kwa barua.

ü  Hajawajibika- anatowcka nyumbani na kumwachia Mangwasha majukumu ya nyumbani.

ü  Nadhifu- alivaa na kubadilisha suti kila uchao.

ü  Mcheshi- akikosckana kazini watu waliteta.

ü  Karimu- alihudumia watu bila uchoyo.

ü  Mwenyc bidii- biashara ya uchuuzi na duka

ü  Mbaraza- mtu wa watu

ü  Mlevi- anakesha vilabuni vya pombe.

 

b). Maudhui ya usaliti yamejadiliwa kwa kina katika Riwaya nzima. Thibitisha

üMtemi Lesulia amesaliti jamii ya Waketwa kwa kuibagua katika ajira inayowaendea Wakule pekee.

ü  Mtemi Lesulia amesaliti nchi kwa kuzorotesha uchumi kupitia ufisadi na sera mbovu

ü Mtemi Lesulia amesaliti uaminifu wa Ngoswe kwa kuwaambia vijana wenzake wavuruge amani wakati wa uchaguzi ili ushindi umwendee Sagilu bila kujali usalama.

ü  Mtemi Lesulia amesaliti hakimu kwa kumnyang'anya cheti na kumfuta kazi licha ya kufanya kazi kulingana na sheria.

ü  Mtemi Lesulia amesaliti imani ya marafiki zake kwa kuwafukuza walipofika kwake kumpa pole kwa kushindwa kwenye uchaguzi.

ü  Sagilu amesaliti jamii ya Waketwa walioishi Matango kwa kushiriki kuchoma makazi yao licha ya kuwa alitaka achaguliwe kama mbunge.

ü  Sagilu amesaliti Mrima kwa kumhonga pesa ili ashiriki ulevi akijua kuwa alimtaka mkewe Mrima mapcnzi.

ü  Sagilu amesaliti Mangwasha kwa kumtembelea akijifanya anajali lakini ndiye alifadhili mumewe Mrima ashiriki ulevi hadi akafutwa kazi.

ü  Sagilu amesaliti anamsaliti mwanaye Mashauri kwa kumnyang'anya mchumba Cheiya.

ü  Sagilu amesaliti Mtemi Lesulia kwa kumhakikishia kuwa kila kitu kiko shwari katika uchaguzi huku akijua kuwa hangeshinda.

ü  Sagilu amesaliti Mtemi Lesulia kwa kuzaa na mkewe Nanzia huku akijifanya rafiki yake

ü  Sagilu amesaliti jamii ya Matuo kwa kuwauzia watoto maziwa yenye sumu bila kujali yangewadhuru vipi.

ü  Cheiya anamsaliti mchuimba wake Mashauri kwa kujihusisha kimapenzi na Sagilu babaye Mashauri.

ü  Nanzia  anasaliti  jamii  ya  Matuo  kwa  kuhodhi  mali  ya  umma  kwa  manufaa  yake binafsi/kuchoma makazi yao ili afaidi ardhi.

ü  Nanzia anasaliti mumewe Mtemi Lesulia kwa kufanya mapenzi na Mhindi na Sagilu

ü  Sagilu amesaliti Mtemi Lesulia kwa kuzaa na mkewe Nanzia huku akijifanya rafiki yake

ü  Cheiya anamsaliti mchuimba wake Mashauri kwa kujihusisha kimapenzi na Sagilu babaye Mashauri.

ü  Nanzia  anasaliti  jamii  ya  Matuo  kwa  kuhodhi  mali  ya  umma  kwa  manufaa  yake binafsi/kuchoma makazi yao ili afaidi ardhi.

ü  Mbwashu  anasaliti  Mtemi  Lesulia  kwa  kumtoroka  na  kwenda  Ulaya  anaposhindwa nawalifanya maovu mengi pamoja.

ü  Chifu Mshabaha anasaliti Waketwa kwa kushiriki njama ya kuwaondoa makao yao.

ü  Chifu Mshabaha anamsaliti Mangwasha kwa kuleta msichana mwingine kazini ili kumfuta yeye kazi.

ü  Mrima anasaliti mkewe Mangwasha kwa kushiriki mapenzi nje ya ndoa/anashirikiana na Sagilu huku mkewe akiteseka.

ü  Mrima anasaliti Mangwasha na akina Lonare anapochukua hongo ili amfanyie Mtemi Lesulia kampeni ilhali anajua huyu ni adui ya Waketwa.

 

2. Matatizo ya Afrika ni tokeo la uongozi mbaya. Thibitisha kwa kurejclea riwaya ya Nguu za Jadi. (alama 20)

ü  Uhab w ajira- vijanwaliokamilishmasom wanakos ajir na   wengine wanaonekana na Mangwasha wakiwa katika maeneo ya maduka wakipitisha wakati.

ü  Kufutwa kazi kiholela- Mangwasha anafutwa kazi bure katika ofisi ya chifu Mshabaha wa kuunga mkono lonare.

ü  Ukiritimba wa kiuchumi- wenye ushawishi kama akina Sagilu wanamiliki nyenzo zote

ü  muhimu za kiuchumi k.v  mashamba, vituo vya petrol na msururu wa maduka ya jumla.

ü  Unyakuzi  wa  ardhi-  Sagilu  na  Lesulia  wanapanga  njama  ya  kunyakua  ardhi  ya Wanamatongo badala ya kuwatetea.

ü  Unyakuzi wa mali ya umma- Nanzia mkewe Mtemi Lesulia ananyakua jengo moja refu katikati ya mji na kubadilisha jina kuwa Skyline Mall.

ü  Ubaguzi-  Utawala  wa  Lesulia  kuajiri  tu  Wakule hata  wale  hawajahitimu  vilivyo  na kubagua Waketwa.

ü  Ukabila- Mshabaha kuajiri watu wengi wa kabila lake

ü  Kunyanyasa wapinzani- magari ya Lonare yanashikwa bila hatia ila ni kwa sababu anampinga Mtemi Lesulia.

ü  Uharibifu wa mazingira- matajiri wanachimba mawe na wengine kumiliki karakana za machimbo ya mawe.

ü  Ufisadi/ hongo- chifu Mshabaha anapokea hongo ili aridhiane na serikali ya Mtemi Lesulia kuinyakua ardhi ya Matango kufuatia misingi ya kisiasa.

ü  Kuchoma nyumba- nyumba za Waketvwa kama vile Mangwasha zinachomwa kwa misingi ya kikabila na kisiasa.

ü  Mishahara duni- Mangwasha anapata mshahara usiokimu familia yake.

ü  Bidhaa ghushi- Sagilu anaagiza maziwa yaliyotiwa sum una kuhatarisha maisha ya watoto wengi.

ü  Biashara haramu- madanguro

ü  Ukosefu wa haki kuamua kesi- Mafamba ni wakili laghai wa serikali- inashinda kesi mbalimbali

ü  Utekaji nyara- utawala wa Lesulia unamteka nyara Lonare ili asishindane naye katika uchaguzi.

ü  Kutumia vijana kuzua vita- Lesulia kuwapa vijana fedha ili wahonge watu siku ya uchaguzi na kuzua fujo katika vituo vya Majengo na Matango ambavyo vilikuwa na ufuasi mkubwa wa Lonare.

ü  Siasa za chuki- Lesulia hakutaka upinzani ndio maana ana chuku kwa Lonare mpinzani wake.

ü  Mfumuko wa bei- bei ya bidhaa muhimu imepanda katika nchi ya Matuo na kuwafanya

ü  watu wa tabaka la chini kama Mangwasha kushindwa kuzimudu.

ü  Ulanguzi wa mihadarati- Ngoswe, mwanawe Mtemi na watu wengine wenye ushawishi wanamiliki mtandao mkubwa wa ulanguzi wa dawa za kulevya na kudhuru afva za wananchi

ü  Ulanguzi wa mihadarati- Ngoswe, mwanawe Mtemi na watu wengine wenye ushawishi

3. “Samahani… Nina shida kidogo. Ninaomba usaidizi. Sikuwa nikilipa ushuru katika biashara zangu. Sasa wanataka kuzifunga na kunipeleka kotini.”

a) Eleza muktadha wa dondoo

ü  Haya ni maneno ya Chifu Mshabaha

ü  Akimwambia Mangwasha

ü  Ofisini mwa Mangwasha mjini

ü  Alikuwa ameenda kumwoba msaada kama angemsaidia kumtetea katika ofisi za kiserikali ahurumiwe kutolipa ushuru na biashara zake zisifungwe.

b) Bainisha toni katika dondoo hili (alama 2)

ü  Toni ya kurai-samahani

ü  Toni ya masikitiko-sasa wanataka kuzifunga na kunipeleka kortini.

ü  Toni ya uoga –naomba usaidizi.

c) Msemaji wa maneno haya na wengine ni adui ya wananchi wa Matuo. Eleza ukweli wa kauli hili. (alama 14)

Chifu Mshabaha

ü  Ufisadi - Chifu Mshabaha na wengine wanapanga kuitwaa ardhi ya mtaa wa Matango kwa manufaa yao wenyewe.

ü Kuwateka nyara wapinzani wa Lesulia-Lonare anatekwa nyara na kupigwa sana siku chache kabla ya uchaguzi na Serikali ya Lesulia.

ü  Uzinzi-Sagilu anashiriki uozo huu na Cheiya.

ü Kuwadhulumu wanawake - Sagilu anamtaka mapenzi Mangwasha akijua tayari amechumbiwa na Mrima na anapomkataa Sagilu anafanya kila juhudi kuismbaratisha ndoa ya hawa wawili.

ü  Kupanga kuwafurusha Waketwa kutoka Matango kwa sababu ya tamaa ya mali na uongozi.

ü Kuwaua watu- Sihaba anatumwa na Sagilu kumwangamiza mwanabiashara mkubwa wa sariji kwa kijana Kifaru-huu ni ukatili.

ü  Kuuza  bidhaa  haramu  na  hatarkwa  wananchi - Sagilu  anaagiza  maziwa  ya  watoto yaliojaa vijasumu ili yasiharibika haraka.Watoto wanapoyatumia wanaathirika sana.

ü  Kupitia kwa Mahauri mtaalamu mkuu wa usanifu wa majengo jijini Taria anaidhinisha ubomoaji wa jingo la Lonare.

ü  Viongozi walichochoea ukabila katika ofisi za umma- Chifu Mshabaha anamfuta kazi Mangwasha kama mhazili wake wa miaka nyingi na kumwandika kazi msichana wa kabila lake.

4. Hivyo, alitaka kubadili hali hata kama ilimaanisha kukitia kichwa chake kinywani mwa samba. Alitaka kuliokoa jahazi lililokuwa likielekea mwambani kwa kasi. Lakini angeliweza vipi kupambana na utandu wa mahasisi hao?

a) Eleza mbinu nne za mimtindozinazojitokeza katika dondoo

ü  Taswira-lililokuwa likielekea mwambani

ü  Jazanda-kukitia kichwa chake kinywani mwa samba

ü  Swali balagha.-lakini angeliweza vipi kupambana na utandu wa mahasidi hao?

ü  Nahau- kuliokoa jahazi

b) Eleza sababu za mrejelewa kutaka kufaulisha kauli iloyopigiwa mstari (al 10)

ü  Ufisadi umekithiri katika nchi ya Matuo. Watu wenye ushawishi kama Sagilu hawakulipa kodi na waliagiza hata bidhaa hatari kama maziwa ya watoto yenye sumu.

ü  Kulikuwa na ukabila - Mangwasha anaeleza jinsi waajiiwa wengi katika ofisi ya chifu walikuwa wa kabila lake mshabaha.

ü  Ubaguzi katika ajira - Utawala wa mtemi unawabagua waketwa wakati wa ajira.

ü  Uhaba wa ajira - Vijana wengi waliokuwa wamehafilika kutoka taasisi za elimu walikosa kazi.

ü  Ukiritimba wa kiuchumi - Sagilu anamiliki nyenzo zote muhimu za kiuchumi

ü  Unyakuzi wa mali ya umma - Nanzia ananyakua jengo moja refu katikati ya mji.

ü  Unyakuzi wa ardhi ya wanajamii - Sagilu napanga kunyakua ardhi ya wanamatango.

ü  Kufutwa kazi kiholela - Mangwasha anapigwa kalamu katika ofisi ya chifu kwa kuunga mkono kampeni za Lonare.

ü  Mshahara mdogo kwa wafanyikazi - Mshahara anaolipwa Mangwasha haukuhudumia familia yake.

ü  Ukosefu wa elimu miongoni mwa vijana - Mangwasha aliwaona vijana wakizurura mtaani.

ü  Kutelekeza watoto wa kiume na kuishia kuingilia matumizi ya dawa za kulevya.

ü  Watoto wa kike wanatumiwa katika biashara ya ngono. Sihaba anamiliki danguro anapotumia wasichana wadogo.

ü  Ulanguzi wa mihadarati - Ngoswe namiliki mtandao wa ulanguzi wa dawa za kulevya.

ü  Matumizi ya pombe haramu - Mrima wanabugia pombe harmu

ü  Ukware. Sagilu anajihusisha kimapenzi na Cheiya ingawa ana mke.

ü  Utekaji nyara. Utawala wa Lesulia unamteka nyara Lonare ili asishindane naye katika uchaguzi.

ü  Uharibifu wa mazingira. - Viongozi walichimba mchanga na kukata miti bila kujali.

c) Eleza umuhimu wa mrejelelewa katika kujenga ploti ya riwaya hii (al 6)

Ngoswe

ü  Mlanguzi wa dawa za kulevya anauza dawa za kulevya hata Lonare anamwambia aache

ü  Mpyaro anamtusi Sagilu   Mzinifu – anamweleza rafikiye Mashauri kuwa hafai kuwa na mpenzi mmoja kama alivyo na Cheiya tu.

ü  Mbadhirifu anasemekana kutumia pesa za kodi anayokusanya kutoka kwa nyumba za babake ovyo

ü  Mpenda anasa – anasemekana kuwa na vilabu vya ulevi. Pia anajihusisha na wasichana wengi vilabuni

(b) Jadili umuhimu wa msemewa wa kauli hii

Mashauri

ü  Anajenga ploti. Anakosana na Cheiya kwa sababu ya usaliti wake.

ü  Anaendeleza maudhui mbalimbali. Anaendeleza maudhui ya mabadiliko kwa jinsi anavyohusiana na babake. Pia anaacha kushirikiana na serikali na kujihusisha na upande wa Lonare.

ü  Anajenga sifa za wahusika wengine. Anajenga sifa za Cheiya kama saliti. Cheiya ambaye ni mpenziwe anamsaliti kwa kujihusisha na babaye.

ü  Anakuza migogoro mbalimbali katika riwaya. Anakuza mgogoro wa kimapenzi, kisiasa n.k.

ü  Anaonyesha namna usaliti unavyoweza kuleta uhasama kati ya watu wa jamii/familia moja. Anakosana na babake kwa kumsaliti na mpenziwe.

ü  Ni kielelezo cha watu ambao wanabadilika kimsimamo wanapotambua makosa yao.

ü  Baada ya kutambua uovu wa serikali ya Lesulia, anajitenga nao na kujiunga na Lonare.

(c) Wanaosemekana kushikana mikono wanaendeleza uozo katika jamii. Thibitisha.

Sagilu na Cheiya

ü  Sagilu anaendeleza ufisadi kwani anauzia watu bidhaa ghushi. Alileta maziwa ya watoto ya viwango vya chini na yenye sumu.

ü  Sagilu anawanyanganya watu wake zao. Wake zake wote walikuwa mabibi za watu.

ü  Sagilu alizini na Cheiya ambaye alikuwa mpenzi wa mwanawe

ü  Sagilu anapata mtoto na Nanzia ambaye ni mke wa mtemi.

ü  Sagilu anataka kuvuruga ndoa ya Mrima na Mangwasha. Alimpa Mrima pesa akasahau majukumu yake.

ü  Sagilu anawalipa watu kwenda kumteka nyara Lonare kwa nia ya kumuua.

ü  Sagilu anahusishwa na kupanga njama ya kuharibu kampeni za Lonare.

ü  Sagilu anahusishwa na uchomaji nyumba za waketwa.

ü  Cheiya anatumwa kumuua Lonare kwa kumwekea sumu katika kinywaji

ü  Cheiya anamsaliti mpenziwe kwa kujihusisha kimapenzi na Sagilu

ü  Cheiya anasemekana nujihusisha na Mashauri kwa sababu ya pesa zake na si mapenzi

(d) Bainisha mtindo katika dondoo.

ü  Kuchanganya ndimi – I say, wajua nimewaona wapi leo?

6. Mandhari ya afisi ya Chifu Mshabaha ni muhimu sana katika riwaya hii ya Nguu za Jadi. Onyesha namna mandhari hayo yanajenga;

(a) Maudhui mbalimbali

ü  Ufisadi chifu halipi ushuru

ü  Hila/njama –kuna watu walipanga njama/mkutano wa siri wa kuchoma nyumba za waketwa

ü  Ubaguzi –chifu anabagua waketwa. Ameajiri wakule wengi katika afisi yake. Mangwasha pekee ndiye mketwa na anafanya majukumu mengi

ü  Ukabila –chifu anamchukia Mangwasha na Mrima kwa kuona kuwa wanaoana   Unyanyasaji/dhuluma –chifu anamdhulumu Mangwasha kwa kumwachisha kazi ovyo

ü  Ubarakala –chifu anafanya kila kitu kumpendeza Mtemi na Sagilu badala ya kuwalinda wananchi

ü  Uwajibikaji Mangwasha anasemekana kuwajibikia kazi yake pale afisini. Hakuzembea.

ü  Ndoa –Mangwasha na Mrima wanapatana pale afisini na kuwa marafiki hadi kuoana/mangwasha anaomba ruhusa ya siku chache pale afisini ili aende kufunga ndoa na Mrima.

ü  Ukatili kuchomea waketwa nyumba


ü  Siasa mbovu/uongozi mbaya afisi ya chifu inaathiri siasa kwani inapanga kumsaidi Sagilu na Mtemi ili wawashide wapinzani wao.

ü  Unyakuzi stakabadhi za kuchangia kesi ya kulinyakua shamba la watu wa matango zilipatikana katika afisi hii

ü  Unafiki –chifu Mshabaha anajidai kuwa wao ni wasamaria wema wa kumwauni Mangwasha ila sivyo

ü  Mapenzi mapenzi baina ya Mrima na Mangwasha yalianzia hapa

ü  Siri mikutano  mingi ya kisiri ilifanyika hapo na Sagilu

 

ü  Usaliti –Chifu Mshabaha anawasaliti wananchi wa eneo lake la kazi kwa kujiunga na wachomaji nyumba za waketwa.

(b) Migogoro ya aina mbalimbali.

ü  Mgogoro wa kikazi/kazini baina ya Mangwasha na Chifu Mshabaha/serikali

ü  Mgogoro wa kikabila baina ya waketwa na wakule

ü  Mgogoro wa  kimapenzi/ mapenzi baina ya Mangwasha, Mrima na Sagilu

ü Mgogoro wa kiutawala baina ya Chifu Mshabaha na serikali kuu kwa kukosa kumhakikishia Sagilu ushindi. Pia baina ya Mangwasha na serikali kwa chifu kumwachisha kazi kwa kujihusisha na upinzani.

ü  Mgogoro wa kikazi/kazini baina ya Mangwasha na Chifu Mshabaha/serikali

ü  Mgogoro wa kikabila baina ya waketwa na wakule

ü  Mgogoro wa  kimapenzi/ mapenzi baina ya Mangwasha, Mrima na Sagilu

ü Mgogoro wa kiutawala baina ya Chifu Mshabaha na serikali kuu kwa kukosa kumhakikishia Sagilu ushindi. Pia baina ya Mangwasha na serikali kwa chifu kumwachisha kazi kwa kujihusisha na upinzani.

ü  Mgogoro wa kimapenzi baina ya Mrima/Mangwasha na Sagilu kupitia kwa chifu. Chifu anamtusi na kumdhihaki Mangwasha kwa kumkataa Sagilu.

ü  Mgogoro wa kisiasa baina ya waketwa na wakule. Chifu anajihusisha katika maswala ya kisiasa ili kuhakikisha Sagilu amechaguliwa.

ü  Mgogoro wakiuchumi kwani inasemekana kuwa Chifu ni miongoni mwa watu wasiolipa ushuru nchini.

7. Yapimeni maneno ya … ‘Hata kama tuna ushahidi huu, tangu lini panya akashinda kesi mbele ya baraza la paka?”

(a) Fafanua muktadha wa maneno haya. (al 4)

ü  Msemaji mangwasha

ü  Msemewa lonare, sagura na mbungulu

ü  Mahali wako kwenye hema la mangwasha/kwa mangwasha

ü  Hii ni baada ya mangwasha kuona kuwa kesi hiyo itakuwa ngumu kwa kuwa mwasisi wake ni mtemi.

(c) Onyesha jinsi akina ‘panya’ walivyonyimwa haki katika riwaya hii.

ü  Kufurushwa wakazi wa matango wanafurushwa kutoka kwao kufuatia sababu za kisiasa.

ü  Kushambuliwa Lonare amekuwa akipangiwa mauaji na viongozi wakule kama vile Mtemi Lesulia ila ameepuka mitego hiyo ya hatari.

ü  Kudhalilisha - Chifu Mshabaha anamdhalilisha mangwasha kwa kumtusi.  Anamwambia kwenda! Waketwa ni watu wasio na akili hata ya kuwachagua wachumba.

ü  Kufutwa kazi mangwasha anafutwa kazi na chifu Mshabaha bila kuwepo kwa sababu maalum.

ü  Kuchomewa nyumba waketwa wanachomewa nyumba zao eneo la matango kwa sababu za kisiasa na wanakosa mahali pa kulala na wanasumbuka kwa baridi.

ü  Kutekwa nyara Lonare anatekwa nyara na Mtemi Lesulia ili kuharibu mpango wake wa kupigiwa kura.

ü  Kuharibu mali yao mashauri analibomoa jengo la Lonare kwa sababu za kisiasa.

ü  Kunyimwa nafasi za ajira Serikali ya Mtemi Lesulia inakosa kuwaajiri vijana Waketwa waliohitimu kwa sababu ya ukabila.

ü  Unyakuzi wa ardhi yao Mtemi Lesulia anayakua ardhi ya Matango ili ampe mke wake Nanzia na Mbwashu kibaraka wake.

ü  Kuhangaishwa na polisi Magari ya Lonare yanashikwa bila sababu na hata madereva wake kushikwa kwa makosa yasiyoeleweka.

8. Ole wako ewe mwanaume uishiye leo. Unaye chakura mapipa ili kuizima njaa uliikosea nini jamii hata usalie kuwa ombaomba? Umevaa koti kuukuu na umesalia kuwa nyuma kama koti hilo. Yu wapi baba aliye kutelekeza? Wapi jamii isiyothamini elimu na utu wako? Jamii ilimshika mkono mtoto wa kike. Ikapiga mbio na mtoto wa kike. Ikasahau kwamba hata wewe unastahili kushikwa mkono. Lazima tujirudi tuone ni wapi tulipoanza kupotea njia. Lazima tuokoe kizazi hiki kinacho potea nyikani bila matumaini. Ole wako matuo, utashika mti gani?

a) Changanua mtindo katika dondoo hili. (alama 10)

ü  Taswira kuchakura mapipa

ü  Swali balagha – usalie kuwa ombaomba?

ü  Tashhisi matuo kushika mti gani.

ü  Majazi matuo – kusonga mbele ambapo nchi ya matuo haisongi mbele kwani inakumbwa na changamoto nyingi mf. Umaskini, ukosefu wa ajira.n.k.

ü  Msemo kushika mkono

ü  Tashbihi/tashbiha – kusalia nyuma kama koti

ü  Uzungumzi nafsi-ole wako matuo utashia mti gani?

b) Juhudi za kuzuia ufanisi wa jamii ni juhudi za mfa maji. Jadili (al 10)

ü  Chifu mshabaha anataka amchagulie Mangwasha mume na amlazimishe aolewe na Sagilu ila Magwasha anakataa na anaolewa na Mrima.

ü  Sagilu alimfahamu na kumdharau sana Mrima ila ndiye anayemuoa Mangwasha ambaye anamkataa mume huyu aliye na mali.

ü  Mbungul anakany Mangwasha   kwenda   Ponda   mali   kumtafut mumewe,   Mrima, aliyepotelea ulevini kwa madai kuwa utamaduni hauruhusu ila Mangwasha anapuzilia mbali utamaduni huo potovu na naelekea huko kumtafuta. (uk.32)

ü  Uongozi wa Mtemi Lesulia unawanyima waketwa kazi ila kuna wale wanaobahatika na kupata ajira katika kampuni za kibinafsi huku wengine wakianzisha biashara zao. (uk.45)

ü  Lonare anawakabili wapinzani wake; Sagilu, Mbwashu, Chifu mshahaba hotelini Saturn na kumkabidhi bahasha yake yenye pesa za hongo.

ü  Lonare Anawaongoza watu wake wa jamii ya waketwa kwa ujasiri licha ya vitisho na mitego ya vifo kutokana na mashambulizi ya watu waliotumwa kumwangamiza.

ü  Lonare alishambulia maovu ya kijamii kwa ukakamavu bila kuogopa serikali dhalimu ya Mtemi Lesulia.

ü  Akiwa kiongozi wa upinzani; Lonare anahujumiwa katika biashara na majengo yake, anatekwa nyara na kuteswa ili asishiriki kwenye uchaguzi ila anashiriki na kushinda kura.

ü  Wakati wa uchaguzi uliopita Lonare alitekwa nyara na kuteswa na hakutetereka akaendelea kuwa mpinzani katika uchaguzi wa sasa.

ü  Lonare hajali ukabila uliopo nchini Matuo na hata anamwajiri mbaji kuwa meneja wa kampuni ya mabasi yake ilhali Mbaji ni Mkule naye ni Mketwa na jamii hizi zilichukiana

ü  Magari yake Lonare ya usafiri yanapokamatwa kwa visingizio visivyokuwa na maana hadi madereva wake kutozwa faini zisizoeleweka, havunjiki moyo bali aliendelea na biashara hiyo.

ü  Lonare anawaelimisha wanawe wote bila ubaguzi wa kijinsia katika jamii hii iliyojaa ubabedume.

ü  Licha ya kuwa kuna ukabila na anaukemea ukabila huku akitaka watu wote watendewe haki.

ü  Lonare anapigania haki kwa waketwa wanaochomewa makazi yao na kufurushwa Matango hasa pale anapoungana na Mangwasha kupeleka kesi mahakamani.

ü  Cheiya alitaka kumuua Lonare wakati mmoja ila akashindwa na Lonare anapomwona, anataka akamatwe kwa kosa hilo.

ü  Cheiya alijaribu kukimbia ila baadaye aliweza kukamatwa na kufikiswa kwenye kituo cha polisi. (uk 156,157)

ü  Sagilu anashiriki na Mtemi Lesulia pamoja na Chifu Mshabaha ardhi ya waketwa eneo la Matango, anaishia kupoteza kura ya ubunge.

ü  Sihaba anafanya biashara ya ukahaba kwa kutumia wasichana wadogo, kupitia Mangwasha na Mrima, watoto hawa wanaokolewa hiyo kufungwa na Sihaba anatiwa mbaroni.  (uk 141,142)

ü  Sihaba alitaka kuwaangamiza Mrima na Mangwasha katika harusi yao, anagundulika na anakimbilia usalama wake na anafaulu kutoweka.

ü  Mangwasha na Mbungulu wanamwona Sagilu akiwa amerukwa kichwa na Mangwasha anasema kuwa ni kutokana na uovu alioufanyia watu ndipo akawa mwendawazimu; ulikuwa msiba wa kujitakia.

9. ‘Habari hizo nimeshazipata tangu juzi. Mwakala wangu hawalali. Wala hayo yasikutie tumbo joto’

a) Weka dondo hili katika mukthadha wake (alama 4)

ü  Haya ni maneno ya Lonare

ü  Anamwambia Mangwasha.

ü  Wakiwa ofisini mwa chifu Mshabaha

ü  Wanazungumzia kuhusu vijikaratasi vilivyo sambazwa ili kuhamisha waketwa.

 

b) Msemaji wa maneno haya anaendeleza vipi maudhui mbalimbali katika riwaya hii? (alama 6)

ü  Dini - Lonareanasema kuwa mlinzi wake ni mungu na wapili ni wafuasi wake.

ü  Uzalendo anawania uongozi ili atetee wananchi.

ü  Utetezi wa haki anashambulia mavua ya jamii.

ü  Bidii anafanya juhudi kuoana watoto wa kike wamesoma

ü  Utu anamtembelea mangwasha ili kumjulia hali.

ü  Malezi anawalea wanawe vizuri.

ü  Mapenzi anawapa wanawe mapenzi ya wazazi wote wawili baada ya mkewe kufariki   Uwajibikaji anawaleta polisi kulinda mali ya wenyeji wa Matango

ü  Siasa angombea kiti cha kua mtemi

c) Eleza jinsi mwandishi alivyotumia mbinu ya sadfa katika riwaya

ü  Ni sadfa Mangwasha kupitia ofisini mwa mrima na kumpata Sagilu.

ü  Ni sadfa kwa wanabiashara kukutana na watuwalioanzisha moto usikui sadfa Sagilu kumtembelea Mangwashawakati ambapo anhitaji kubwa la pesa kuwanunulia mawnawe sare

ü  Ni sadfa Mangwasha kupata dirisha ambalo halikungwa kanisani

ü  Sadfa inawakutanisha Mrima na Magwasha katika ofisi ya chifu na kuanza kuchumbiana

ü  Ni sadfa kwa sukari, chumvi na mafuta kuisha pamoja mwezi unapokariba

ü  Waketwa wanapiga gari la sihaba msako na kupata vijikaratasi vya kuwahamisha

ü  Ni sadfa mbungulu kumtembelea rafikiye kisha anapata zilipo Red Bead Lodgings.

ü Lonare anatekwa nyara siku ambayo walinzi wanaacha kumlinda

ü  Ni sadfa Lonare kupatikana siku ya kupiga kura

Get this full document in Pdf Format